Pages

Subscribe:

ContactMe

Friday, July 19, 2013

OBI, MBWA 'MTUMISHI' ALIYEBADILI MAISHA YA JAMII KUMFUATA YESU


Hakika ni ajabu ukisikia, na hata ukiona ndio utashangaa zaidi – utashangaa kuona kuwa hata mbwa anatumiak kuvuta watu kanisani, na kuwapa faraja katika Kristo Yesu, na hatimaye kujifunza zaidi kuhusu Mwokozi Yesu na kumpokea. Ndivyo ilivyo kwa kanisa la Kreutz Creek Presbyterian lililopo Pennsylvania nchini Marekani lilivyojaliwa Neema ya pekee.


Mchungaji Marion Haynes-Weller anaeleza namna ambavyo mambo yalikuwa wakati wa mahojiano na Christian Post, “Tulikujua kwamba tuna kuna watoto kwenye hii mitaa yetu, na tulikuwa tukiwaona na kuwapungia mkono, lakini wengi wao sio watu wa kanisa – yaani wamejitenga na kanisa, hivyo inakuwa tabu unapoanza kumfuata kwa lengo la kumhubiria, na hawakuwa wanapenda”
Kanisa hilo ambalo lipo kwenye mji wenye takriban watu elfu sita, Hellam, York, sasa linabadili historia ya mji huo kutokana na namna ambavyo mitaa inabadilishwa kiimani, kutokana na Obi, mbwa ambaye amekuwa kivutio kwa watoto na wakazi wa jamii hiyo.
 
“NIlianza kuja naye kipindi akiwa mdogo hapa kanisani, hapo watoto walianza kukaa na kucheza nae.
Baada ya hapo nikawa namleta karibu kila Jumamosi kwenye ibada yetu ya usiku, lakini bado alikuwa mdogo sana kwahiyo watu wakawa pia wanakuja kumuona” Anaeleza mchungaji Haynes namna ambavyo mbwa huyo aliingia kwenye huduma yake. 
 
Kadri Obi alizidi kukua, ndivyo ambavyo alianza kuona tofauti ya mwenendo wake kwa watu ambao aliwavutia kuja kanisani.
Mch. Haynes, ambaye mume wake ni mwanasaikolojia mwenye paka anayefanya kazi ofisini kwao alikuwa pia hamasa kwake na kupelekea kugundua faida ya kuwa na mbwa huyo kwenye maeneo ya kazi yake ya utumishi, kwa kuwa anaweza kuwafanya watu wenye wakati mgumu angalau kupumua, nah ii sio kwa watoto tu, bali hata watu wazima.
Unajua watoto wakiwa kama wanataka kujakukaangalia ka-mbwa, mimi huwa nawaambia eeh karibuni mbwa yupo, basi mwanzoni ilikuwa ni watoto wachache, lakini sasa hivi imehamasisha watoto wa mtaa wote mara tu walipojua kuhusu taarifa hizi.
 
 Darasa likiendelea, mchungaji Haynes akiwa na Obi kwenye mafundisho picha kupitia Screen Grab via Daily Record/Sunday News


Mtazamo wa kanisa hili hivisasa umebadilika, yaani kutoka sifuri hadi kaya zaidi ya 20 ambazo sasa wankuja kanisani. Na si kwa watoto tu, hata walewatu wazima wasio na watoto nao huja kujumuika kwa pamoja na mbwa wao, jambo ambalo limeongeza idadi ya washiriki kanisani hapo, ambao kidogokidogo huubiriwa injili, ijapokuwa hawakuwa wanakuja kanisani mwanzoni.
Lakini katika hatua nyingine, Obi ameonekana msaada kwa watoto wasiojua lugha ya Kiingereza, ama kwa wale ambao kwao ni lugha ya pili. Kwani wasipokuwa na mtu wa kuongea, Obi anaweza kuzungumza nao, wanazungumza “dog language”
, ambayo karibu kila mtoto anaielewa.
Kanisa hilo kwa hivi sasa linaendesha mafunzo katika kipindi cha likizo, ‘Vacation Bible School Obi’, ambapo watoto wenye umri wa kuanzia miaka 6-14 wamepata fursa ya kuhubiriwa kuhusu Yesu, ambpo hapo awali hawakujua A wala B kuhusu hadithi za Biblia.
“Siku moja tulikuwa nje tunacheza na mbwa, na nikasema – unajua tunaweza kukaa na kupanga mikakati, nitawapa chakula na tutakuwa na maombi” Anaeleza Mchungaji Haynes na kasha mtoto mmoja akamuuliza, “maombi ni nini?” Akajibu “ni pale unapozungumza na Mungu”. Kisha mtoto mwingine akauliza, Mungu ni nani?
“Kuanzia hapo tukaanza sifuri, na hivi sasa watoto wanakuja na kuomba, na kufahamu hadithi za Biblia, kwa kuwa hawaijui kwani kuna siku walikuw wanaigiza kuhusu Musa, na hakuna akati yahao watoto aliyekuwa anmjua Musa ni nani, wengi walishamsikia Yesu, lakini Musa hakuwa akilini mwao.” Mchungaji Haynes anasema na kumalizia kwa kicheko kwamba, “Yaani saivi wanaombeana wenyewe kwa wenyewe na pia wanaombewa. Ni jambo jema kuona Mungu anatenda kupitia vitendea kazi tulivyo navyo, na muda huu kitendea kazi ni 80lb Labrador (aina ya mbwa).
Hakika ya Mungu ni mengi, chochote kinaweza kutumika kumhamasisha mtu kufika kanisani, ama kwenye kusanyiko lenye injili kuhubiriwa, na basi kwa mahali ulipo pia, unaweza kutazamia ni kitu gani kinaweza kuwapa hamasa watu kufika – ili wapata kumjua Yesu Kristo. Na katika yote,m tufanye kwa imani.
 
CHANZO: gospelkitaa.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment